Elimu ya mahaba

simulizi za kusisimua

KILA DEMU NA UTAMU WAKE

Watu waliomjua tangu akiwa na umri wa miaka 17 walidhani huenda ni umri unaomsumbua. Wakaamini kwamba atakapokuwa mtu mzima angeacha, haikuwa hivyo kwani kila siku, Boi ambaye jina lake halisi ni Lawrence Godfrey aliwabadili wanawake wa kila rika kama daladala zinavyopishana barabarani.
Mwanamke gani amtongoze na kumkosa? Sketi gani nzuri ipite mbele yake bila kuingia mikononi mwake? Jambo hili liliwafanya rafiki zake wajue kabisa huenda Boi anatumia dawa za kuwatia kiwewe wanawake wazidi kumpenda.
Kila rangi ya mwanamke, mwenye sifa za uzuri, Boi aliweza kumgusa na kuona mwisho wa raha zake.
Katika daftari lake la kumbukumbu za wasichana aliotembea nalo lilijaa, jambo ambalo lilimtisha sana rafiki yake aitwaye Dullah!
“Kaka, hivi unatumia kinga?” Dullah akavunja ukimya.
“Natumia kaka, kwani umeshawahi kusikia nina mtoto sehemu?”
“Hapana, ila punguza bwana…”
“Najaribu kupunguza nashindwa, wanawake wanatofautiana sana, ukikutana na huyu anaguna, mwingine analia, mwingine anacheka, mwingine ananyamaza kimya. Nakuambia ukweli, yupo mwingine anapiga kelele hadi mtaa wa tatu wanasikia.Tangu nimewajua, nimegundua wako tofauti kuliko watu wanavyofikiri…”
“Hapo napo kweli, lakini unawajuaje?”
“Kuwajua ni hapo unapokuwa nao kitandani…”
“Duh! Unajua sielewi kabisa.”
“Poa, hunielewi acha nikueleweshe.Ngoja nikuulize swali.”
“Uliza.” Dullah akadakia, akitega sikio vema.
“Hivi, sikio langu na lako lipo sawa?” Boi akamuuliza Dullah.
“Hapana, sikio langu refu kidogo na limepinda kama sikio la Popo, lakini lako dogo na limesimama kama la sungura…”
“Mmmh! Hata wanawake katika maumbo yao yametofautiana, mimi na wewe ni wanaume lakini tupo tofauti, unalijua hilo?”
“Nafahamu!”
“Mimi huenda Boi mkubwa kuliko Dullah!”
“Kabisa!”
Wakati wanajadili suala la mademu kutofautiana, simu ya Boi ikaanza kuita, akaitazama na kuachia tabasamu pana lililoshiba midomoni mwake.Hawakuwa sehemu nyingine isipokuwa chumbani kwa Boi wakipeana darasa la mahaba.
Getho la Boi lilikuwa maeneo ya Mwenge jijini Dar es Salaam karibu kabisa na Hospitali moja binafsi. Boi ni mwanafunzi mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akiwa anasomea biashara. Dullah naye ni mwanafunzi wa chuo hicho hicho, mwaka wa pili. Ajabu ni kwamba pamoja na Dullah kumzidi daraja la elimu, Boi ndiye aliyefahamika zaidi kutokana na tabia yake ya kupenda na kupendwa na wanawake.
Simu iliendelea kuita, na wakati huu Boi aliwaza jibu gani ampe msichana huyo, siku hiyo alishawaahidi wasichana wawili na wote alipanga kulala nao kwa zamu. Matha hakuwa kwenye ratiba kabisa ya siku hiyo.
“Sikiliza, anapiga Maimatha…,” Boi alimbonyeza Dullah!
“Matha, huyu wa IFM!”
“Haswaa, sijui ni mwambie vipi, maana hapa nimeshaongea na Janeth, anakuja getho ili nimpe dawa.”
“Dawa gani?” Dullah alitaharuki, inamaana Boi ameshakuwa daktari?
“Hujui kuwa Janeth amesema anajisikia mgongo unamuuma sana, hivyo lazima nimnyooshe kidogo na kumpa dozi murua?” Alipotoa kauli hiyo, Dullah akacheka sana.

“Hivi unawezaje kutembea na wasichana wengi kiasi hicho bila kuwagonganisha?”
“Akili kaka, naenda na muda na uongo wangu kamwe sisahau. Pamoja na kuwa bingwa wa kuwachanganya, sitasahau gemu moja gumu. Siku moja nilikuwa na kiu sana, nikamuita Naomi aje saa nne ili saa sita nimuondoe na kumleta mwingine. Nikapanga miadi na Leila yule mtoto wa kigogo wa Bandari kuwa aje saa nane, kwasababu niliamini huenda wasingefika na ningekosa nikaongea na Mei kuwa siku hiyo ningelala naye getho kwangu.



Ajabu nilishapanga tena mechi na Richael, huyu dada ana duka la nguo Kariakoo mtaa wa Kongo kuwa usiku ningekutana naye anipe mautamu kabla ya kulala na Mei.
Sasa kwa bahati mbaya wote wakaja kwa wakati uliokaribiana sana na hapo ndipo balaa. Naomi alifika saa saba na nusu, na Leila anakaja saa nane, Mei naye aliwahi akidai anatamani tuwe pamoja kuanzia mchana hadi usiku, bila kunipigia simu akatia timu. Unaambiwa niliwapanga na kupiga chenga za Messi, kwanza aliyechelewa alipokaribia kufika akanipigia nikamwambia nimetoka kidogo baada ya kumsubiri sana, nikamtaka anisubiri baa ya jirani…ilibidi afanye hivyo. Leila aliyeenda na ‘time’ ikabidi nianze kumshughulikia haraka sana…waaaacha kabiiiisaa!”
“Uligawa vipi muda?”
“Sikiliza, simu yangu kwanza haina sauti na hata ninapokuwa na mwingine sipokei kabisa na kama niliamua kupokea basi niliongea kwa mafumbo kiasi cha kutoshtukiwa kama naongea na mwanamke…”
“Ehee…”
“Baada ya kucheza mechi ya muda mfupi na kuhakikisha kwamba wote tumefunga bao, nilimwacha na kwenda kwa mwingine na yule kumtelekeza chumbani.”
“Baadaye niligundua nimezidiwa na ili niwaweze, nikampigia rafiki yangu Frank kuwa amtulize hotelini nakuja, unaambiwa niliwapanga kama nyanya sokoni na kila mtu alipata dawa.”
“Dah! Boi, punguza bwana…”
“Nishakuambia, sijui ni laana au vipi, kila siku watoto wazuri wanazaliwa, na wote ni wazuri kuliko wa jana…”
“Mikorogo tu hiyo kaka,” Dullah akashusha pumzi baada ya kuwaponda.

kila demu na utamu wake

kila demu na utamu wake
... kila demu na utamu wake..

mara...

Simu ya Maimatha ilipokelewa, tena bila wasiwasi, Boi akamwambia kuwa amelimisi sana penzi lake.
“Weka loudspeaker!” Dullah alimnong’oneza sikioni Boi.
“Yaani, Boi…sijui nisemeje, nakupenda sana na juzi ulinichanganya, kila nikikumbuka naona heri nikuone…”
“Darasani leo umeingia?” Boi akauliza, hakutaka kukutana na mrembo huyo, alikuwa na miadi na Janeth, hivyo aliogopa kufumaniwa.
“Nimeingia kipindi cha asubuhi tu, dear…uko wapi?”
“Nipo maeneo ya Mwenge ila nataka kwenda Sinza.”
“Basi, nisubiri hapo kwako,” Maimatha alisema kwa sauti ya chini iliyojaa pumzi za mahaba.
“Nipo na Dullah, tumepitia saluni kunyoa,” Boi alitania akimbonyeza Dullah.
“Unanyoa nini?”
“Ndevu…”
“Hapana dear, usinyoe…nazipenda sana ndevu zako my darling. Mbona unataka kunitesa?”
“Acha nizinyoe washikaji wananicheka sana wananiita Osama, wengine kidevu.”
“Sikiliza Boi, usinyoe nitakupa elfu hamsini, kweli.”
“Sawa, unakuja?”
“Sasa hivi, nataka leo unipe mapenzi ya juzi, umesikia D wangu…”
“Ndiyo, nitakupandisha nitakushusha, utafurahi…,”
“Sawa, ngoja nikaache gari langu likiendelea kuoshwa kisha naja,” alisema Maimatha kwa sauti iliyojaa michujo ya mahaba. Sifa za mrembo huyu, alikuwa mrefu na mnene kiasi aliyebarikiwa wowowo la nguvu ambalo liliwacha wanaume wengi vinywa wazi alipopita mbele yao.

... inaendelea ndani ...

kilademu na utamu wake

kilademu na utamu wake
... na utamu wake..

Jumatano, 18 Novemba 2015

KUHUSU ZUBAGY AKILIMIA

zubagy akilimia, ni mwandishi wa simulizi za kusisimua, mikasa na habari pendwa nchini Tanzania. Alizaliwa katika kijiji cha Kifaru wilayani Mwanga, akitoka katika ukoo wa Msuya. Baba yake mzee Juma A. Msuya amekuwa akivutiwa sana na kijana wake kutoka na kipaji alichokuwa nacho tangu utotoni, kwani licha ya kupenda kuchora na kuandika simulizi za mahaba, ni mtu aliyejawa vipaji vingi.