simulizi za kusisimua
KILA DEMU NA UTAMU WAKE
Watu waliomjua tangu akiwa na umri wa miaka 17 walidhani huenda ni umri unaomsumbua. Wakaamini kwamba atakapokuwa mtu mzima angeacha, haikuwa hivyo kwani kila siku, Boi ambaye jina lake halisi ni Lawrence Godfrey aliwabadili wanawake wa kila rika kama daladala zinavyopishana barabarani.
Mwanamke gani amtongoze na kumkosa? Sketi gani nzuri ipite mbele yake bila kuingia mikononi mwake? Jambo hili liliwafanya rafiki zake wajue kabisa huenda Boi anatumia dawa za kuwatia kiwewe wanawake wazidi kumpenda.
Kila rangi ya mwanamke, mwenye sifa za uzuri, Boi aliweza kumgusa na kuona mwisho wa raha zake.
Katika daftari lake la kumbukumbu za wasichana aliotembea nalo lilijaa, jambo ambalo lilimtisha sana rafiki yake aitwaye Dullah!
“Kaka, hivi unatumia kinga?” Dullah akavunja ukimya.
“Natumia kaka, kwani umeshawahi kusikia nina mtoto sehemu?”
“Hapana, ila punguza bwana…”
“Najaribu kupunguza nashindwa, wanawake wanatofautiana sana, ukikutana na huyu anaguna, mwingine analia, mwingine anacheka, mwingine ananyamaza kimya. Nakuambia ukweli, yupo mwingine anapiga kelele hadi mtaa wa tatu wanasikia.Tangu nimewajua, nimegundua wako tofauti kuliko watu wanavyofikiri…”
“Hapo napo kweli, lakini unawajuaje?”
“Kuwajua ni hapo unapokuwa nao kitandani…”
“Duh! Unajua sielewi kabisa.”
“Poa, hunielewi acha nikueleweshe.Ngoja nikuulize swali.”
“Uliza.” Dullah akadakia, akitega sikio vema.
“Hivi, sikio langu na lako lipo sawa?” Boi akamuuliza Dullah.
“Hapana, sikio langu refu kidogo na limepinda kama sikio la Popo, lakini lako dogo na limesimama kama la sungura…”
“Mmmh! Hata wanawake katika maumbo yao yametofautiana, mimi na wewe ni wanaume lakini tupo tofauti, unalijua hilo?”
“Nafahamu!”
“Mimi huenda Boi mkubwa kuliko Dullah!”
“Kabisa!”
Wakati wanajadili suala la mademu kutofautiana, simu ya Boi ikaanza kuita, akaitazama na kuachia tabasamu pana lililoshiba midomoni mwake.Hawakuwa sehemu nyingine isipokuwa chumbani kwa Boi wakipeana darasa la mahaba.
Getho la Boi lilikuwa maeneo ya Mwenge jijini Dar es Salaam karibu kabisa na Hospitali moja binafsi. Boi ni mwanafunzi mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akiwa anasomea biashara. Dullah naye ni mwanafunzi wa chuo hicho hicho, mwaka wa pili. Ajabu ni kwamba pamoja na Dullah kumzidi daraja la elimu, Boi ndiye aliyefahamika zaidi kutokana na tabia yake ya kupenda na kupendwa na wanawake.
Simu iliendelea kuita, na wakati huu Boi aliwaza jibu gani ampe msichana huyo, siku hiyo alishawaahidi wasichana wawili na wote alipanga kulala nao kwa zamu. Matha hakuwa kwenye ratiba kabisa ya siku hiyo.
“Sikiliza, anapiga Maimatha…,” Boi alimbonyeza Dullah!
“Matha, huyu wa IFM!”
“Haswaa, sijui ni mwambie vipi, maana hapa nimeshaongea na Janeth, anakuja getho ili nimpe dawa.”
“Dawa gani?” Dullah alitaharuki, inamaana Boi ameshakuwa daktari?
“Hujui kuwa Janeth amesema anajisikia mgongo unamuuma sana, hivyo lazima nimnyooshe kidogo na kumpa dozi murua?” Alipotoa kauli hiyo, Dullah akacheka sana.
“Hivi unawezaje kutembea na wasichana wengi kiasi hicho bila kuwagonganisha?”
“Akili kaka, naenda na muda na uongo wangu kamwe sisahau. Pamoja na kuwa bingwa wa kuwachanganya, sitasahau gemu moja gumu. Siku moja nilikuwa na kiu sana, nikamuita Naomi aje saa nne ili saa sita nimuondoe na kumleta mwingine. Nikapanga miadi na Leila yule mtoto wa kigogo wa Bandari kuwa aje saa nane, kwasababu niliamini huenda wasingefika na ningekosa nikaongea na Mei kuwa siku hiyo ningelala naye getho kwangu.
Ajabu nilishapanga tena mechi na Richael, huyu dada ana duka la nguo Kariakoo mtaa wa Kongo kuwa usiku ningekutana naye anipe mautamu kabla ya kulala na Mei.
Sasa kwa bahati mbaya wote wakaja kwa wakati uliokaribiana sana na hapo ndipo balaa. Naomi alifika saa saba na nusu, na Leila anakaja saa nane, Mei naye aliwahi akidai anatamani tuwe pamoja kuanzia mchana hadi usiku, bila kunipigia simu akatia timu. Unaambiwa niliwapanga na kupiga chenga za Messi, kwanza aliyechelewa alipokaribia kufika akanipigia nikamwambia nimetoka kidogo baada ya kumsubiri sana, nikamtaka anisubiri baa ya jirani…ilibidi afanye hivyo. Leila aliyeenda na ‘time’ ikabidi nianze kumshughulikia haraka sana…waaaacha kabiiiisaa!”
“Uligawa vipi muda?”
“Sikiliza, simu yangu kwanza haina sauti na hata ninapokuwa na mwingine sipokei kabisa na kama niliamua kupokea basi niliongea kwa mafumbo kiasi cha kutoshtukiwa kama naongea na mwanamke…”
“Ehee…”
“Baada ya kucheza mechi ya muda mfupi na kuhakikisha kwamba wote tumefunga bao, nilimwacha na kwenda kwa mwingine na yule kumtelekeza chumbani.”
“Baadaye niligundua nimezidiwa na ili niwaweze, nikampigia rafiki yangu Frank kuwa amtulize hotelini nakuja, unaambiwa niliwapanga kama nyanya sokoni na kila mtu alipata dawa.”
“Dah! Boi, punguza bwana…”
“Nishakuambia, sijui ni laana au vipi, kila siku watoto wazuri wanazaliwa, na wote ni wazuri kuliko wa jana…”
“Mikorogo tu hiyo kaka,” Dullah akashusha pumzi baada ya kuwaponda.
kila demu na utamu wake

... kila demu na utamu wake..
mara...
Simu ya Maimatha ilipokelewa, tena bila wasiwasi, Boi akamwambia kuwa amelimisi sana penzi lake.
“Weka loudspeaker!” Dullah alimnong’oneza sikioni Boi.
“Yaani, Boi…sijui nisemeje, nakupenda sana na juzi ulinichanganya, kila nikikumbuka naona heri nikuone…”
“Darasani leo umeingia?” Boi akauliza, hakutaka kukutana na mrembo huyo, alikuwa na miadi na Janeth, hivyo aliogopa kufumaniwa.
“Nimeingia kipindi cha asubuhi tu, dear…uko wapi?”
“Nipo maeneo ya Mwenge ila nataka kwenda Sinza.”
“Basi, nisubiri hapo kwako,” Maimatha alisema kwa sauti ya chini iliyojaa pumzi za mahaba.
“Nipo na Dullah, tumepitia saluni kunyoa,” Boi alitania akimbonyeza Dullah.
“Unanyoa nini?”
“Ndevu…”
“Hapana dear, usinyoe…nazipenda sana ndevu zako my darling. Mbona unataka kunitesa?”
“Acha nizinyoe washikaji wananicheka sana wananiita Osama, wengine kidevu.”
“Sikiliza Boi, usinyoe nitakupa elfu hamsini, kweli.”
“Sawa, unakuja?”
“Sasa hivi, nataka leo unipe mapenzi ya juzi, umesikia D wangu…”
“Ndiyo, nitakupandisha nitakushusha, utafurahi…,”
“Sawa, ngoja nikaache gari langu likiendelea kuoshwa kisha naja,” alisema Maimatha kwa sauti iliyojaa michujo ya mahaba. Sifa za mrembo huyu, alikuwa mrefu na mnene kiasi aliyebarikiwa wowowo la nguvu ambalo liliwacha wanaume wengi vinywa wazi alipopita mbele yao.
... inaendelea ndani ...
kilademu na utamu wake

... na utamu wake..
Jumatano, 18 Novemba 2015
KUHUSU ZUBAGY AKILIMIA
zubagy akilimia, ni mwandishi wa simulizi za kusisimua, mikasa na habari pendwa nchini Tanzania. Alizaliwa katika kijiji cha Kifaru wilayani Mwanga, akitoka katika ukoo wa Msuya. Baba yake mzee Juma A. Msuya amekuwa akivutiwa sana na kijana wake kutoka na kipaji alichokuwa nacho tangu utotoni, kwani licha ya kupenda kuchora na kuandika simulizi za mahaba, ni mtu aliyejawa vipaji vingi.
Jumanne, 26 Agosti 2014
MAFIA WA BONGO (1)
Mwandishi, Zubagy
Akilimia, 0712313191
Ukimuona kwa jinsi alivyo unaweza
kusema si Mtanzania halisi, hii ilitokana na urefu wake wa futi saba kasoro na weusi uliopitiliza. Kwa
kumtazama ungeweza kusema ni Mkikuyu kutoka Kenya au rai wa nchi jirani ya Rwanda.
Pamoja na kwamba alikuwa na umri wa miaka 17, ungemkisia kwa kusema ana miaka
30. Umbo lake liliweza kutisha wanaume wengi wavimba mbavu mbili na kuwavutia
wasichana wenye kupenda mwanaume mwenye mwili mkubwa.
Kijana huyu jitu la miraba
mnne alizaliwa Tarime vijijini na kukulia huko huko Mkoani Musoma.
Wakati anazaliwa alikuwa
na kilo gramu nne na nusu(kg 4.5).Mtoto huyu kwanza alichelewa sana kutembea na
hata kuongea, wazazi wake awali walidhani wamepata mtoto bubu na mlemavu, haikuwa
hivyo kwani baadaye akiwa na miaka miwili aliweza kutembea na kuongea vizuri
Kikuria.
Utaalamu wake mkubwa, ni kupiga shabaha na ujuzi wa
kuzaliwa nao ulikuwa kukarabati bunduki aina ya ‘Gobole’ na Bastola aina zote
na hata ‘Machine Gun’.
Watu wengi wanafahamu wazi watu wanaoweza kutengeneza au
kukarabati bunduki mara nyingi ni waliopitia mafunzo wa kijeshi, kwa upande wa Masato
Lwegambura watakuwa wamekosea.
Kijana huyu si miongoni mwa watu waliopitia jeshi, ingawa
alitisha na kuonekana zaidi ya mtu aliyepitia mafunzo ya jeshi. Huu ni uwezo
binafsi uliowashangaza hata askari waliokuwa wakimtafuta kwa ajili ya kumtia
mikononi mwa polisi.
Wengi walihisi huenda anatumia dawa za kichawi, kutokana
na uwezo wake wa kuua na kutokomea bila kukamatwa.
Unaweza kujiuliza kichwani mwako.Je, huyu kijana mdogo
ameweza kupata wapi ujuzi wa kukarabati, kutengeneza silaha na kuzitumia, sasa
ukakuna kichwa na kuguna. Mhh!.
Ukweli, historia ya Masato ni nzito sana, ni kijana aliyelelewa
na babu yake mzee Simon Lwegambura, baada ya baba na mama yake kuvamiwa na
kuuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kuchoshwa na ujambazi wa baba yake.
Kifo hicho ndicho kilichosababisha Masato kuwa yatima na kutowafahamu wazazi
wake. Babu yake alimchukua mjukuu huyu na kwenda naye kijiji cha mbali na mjini,
awali familia ya Lwegambura ilikuwa ikiishi Musoma mjini maeneo ya Mwembeni.
Masato akiwa na umri wa miaka mitatu aliishi kiseja na babu yake ambaye hakuwa
na mke wala mtu mwingine wa kumsaidia. Aliishi na Masato akimpikia uji, maziwa
ya Ng’ombe maana alikuwa mfugaji mkubwa wa Ng’ombe.
Kutokana na ukorofi wa mzee Simon Lwegambura, hakuna
jirani aliyekuwa anamsogelea, mara nyingi marafiki zake walikuwa viongozi wa
nchi jirani na matajiri ambao walifika nyumbani kwake asubuhi sana au usiku
wakiwa na magari.
Hakuna aliyeelewa mzee Simon alikuwa akifanya biashara
gani na viongozi na matajiri hao. Kuna watu walianza kusema huenda mzee Simon
ni mpelelezi maana hata magari ya vigogo yalifika kwake na kuondoka. Tetesi
zikaenea mtaani, na kumfanya Mzee Simon aigopwe sana kijijini kwao. Wageni
mbalimbali ambao hawakujulikana walikotoka walifika na kuondoka kisha kurudi
tena na kilichowashangaza wengi ni ile hali ya mgeni kuwa lazima akienda arudi
tena.
Kilichomsaidia watu wengi kushindwa kumuelewa kazi halisi
ya Mzee Simon, ni kule kutopenda kuzoeana na hata wazee wenzake. Zaidi ya
salamu, hakuna mazungumzo mengine.
Ufinyu wa kutozoeana ukazidi kuwatia watu wasiwasi,
wengine walimuona huenda ana uwendawazimu kama si laana.
“Haiwezekani mnaishi na mtu hata hana mazoea wala haendi
kwa mtu, yeye rafiki zake ni wageni…” Mzee mmoja alilalamika, akajaribu
kujipendekeza akachoka maana mzee Simon hakutaka mazoea.
Rafiki yake mkubwa mzee Simon ni mjukuu wake, hata
alipoanza shule ya msingi, majirani na watu mbalimbali walianza kumchunguza
Masato na kutaka kujua ukweli wanavyoishi na babu yake.
“Masato, nyumbani nani anakupikia chakula?”
“Chakula, tunapika na babu…”
“Ahaa! Kwa hiyo hakuna mtu anayeishi na ninyi?”
“Hakuna tupo wawili tu…”
“Safi sana, na wale wageni wanaokuja na kuondoka wanaleta
nini au wanakuja kuchukua nini?” Huyu alikuwa ni mjumbe wa nyumba kumi aliamua
kumfuatilia Masato shuleni.
“Hakuna kitu, wale ni ndugu zetu…”
“Ahaa, mbona wanakuja na kuondoka hawalali?”
“Hakuna nafasi ya kulala, sisi tuna vitanda viwili tu…”
“Sawa, babu yako anafanya kazi gani ndani?”
“Hana kazi, anapenda kusuka ukili tu…” Masato
alidanganya, kumbe mzee huyu ambaye ni mjumbe hakujua kama Masato alishapewa
elimu na babu yake kuhusiana na watu watakaotaka kumpeleleza.
Akili yake ilishalifahamu hilo mapema ndiyo maana
alimfundisha maisha ya ukubwa na jinsi ya kujibu maswali na hata kujitetea.
Baada ya kupeleleza huo wa muda wa dakika kumi, hatimaye
Masato alienda shuleni na kuingia darasani. Hata hivyo, pamoja na kuwa darasani
akimsikiliza mwalimu kwa makini, somo la babu yake ndilo alilolipenda zaidi
kuliko la darasani.
Akiwa na umri wa miaka kumi na moja, darasa la tano
Masato alishafahamu kusafisha bunduki maarufu kwa jina la ‘Gobole’, Bastola za
kila aina, mfano Revolver, M92 Beretta, Short Machine Gun(SMG) nk. Alipofikisha
umri wa miaka 13, babu yake ambaye kazi yake kubwa ilikuwa kukarabati na kutegeneza
silaha kwa siri bila jeshi la polisi kufahamu, alimfundisha ufundi wa
kukarabati silaha zote.
Kutokana na kuipenda kazi hiyo na kupenda kutumia bastola,
Masato akawa mtaalam na hata zilipoletwa bastola za kusafisha na kutengeneza
aliweza kuifanya kazi hiyo kwa ubora wa hali ya juu. Babu yake alishangaa sana
na upendo kwa mjukuu wake ukaongezeka maradufu. Akili mwake, alifahamu amepata
mrithi wa kazi yake, jambo lililompa faraja.
“Umesikia mjukuu wangu, hii ni kazi ninayoifanya kwa
magendo, sipendi mtu yoyote ajue zaidi ya wateja wangu,” ilikuwa sauti ndogo
huku akimshika kichwa na kuchezea nywele zake.
“Nimekuelewa babu, na ukweli babu hii kazi naipenda sana.”
“Nashukuru kusikia hivyo. Ila nakuonya…usije kuiga kazi
ya baba yako…”
“Kazi gani?” Masato akamwangalia babu yake kwa udadisi.
Hakujua kama baba yake alikuwa jambazi sugu na Mafia wa Bongo.
“Baba yako alikuwa jambazi hatari sana Tanzania hii,
nilipenda awe mwanajeshi kwa ajili ya kutetea rai na aridhi yetu ya Tanzania,
kumbe alipokwenda jeshi alienda kwa nia ya kujifunza uwezo wa kuua, kutumia
silaha za kivita na ufundi mwingine wa shabaha…”
“Dah! Baba yangu alikuwa Mafia! Kama akina Van Damme,
Bruce Lee?”
“Zaidi, kwani Van Damme na Bruce Lee walikuwa wanaigiza
filamu tu…yeye alikuwa anafanya kweli, akisema naua leo lazima aue kweli,
akisema navamia duka na kupora pesa lazima afanye hivyo,” yale mazungumzo
yalimvutia sana Masato bila mzee Simon kuelewa kuwa alikuwa anamharibu mjukuu ubongo
wake. Alipenda sana kutumia bastola kuliko kiumbe yoyote duniani.
Kadri siku zilivyozidi kwenda, umri wa babu ulizidi
kumtupa, kazi nyingi zilikuwa zinafanywa na Masato. Kitu kikubwa ambacho
kiliwashangaza majambazi wengi, ni ile hali ya shabaha na uelewa wa kutengeneza
bunduki kwa kutumia miti na vyuma.
Kuna wakati majambazi wa Mwanza wa Kundi la Jembe
walifika Tarime kwa ajili ya kumuomba Masato aweze kujumuika nao. Kijana huyu
aligoma kabisa, maana alipewa historia ya kifo cha baba yake.
Hata hivyo, alipenda sana kutumia bastola na ataitumia
wapi, kama siyo kwenye matukio ya ujambazi? Hili lilikuwa ni zoezi gumu sana
kwake.
“Babu, naomba unifundishe ujuzi mwingine maana naona wewe
sasa hivi umezeheka sana…” Masato akiwa na miaka 17 alimweleza babu yake.
“Kitu ambacho nimekuwa sijakufundisha ni kutengeneza
baruti na mabomu ya kutupa kwa mkono, na itabidi ufahamu vitu vya kutengenezea
na adhari zake kabla ya kuanza zoezi. Itabidi twende msituni ili kunifundishe
zaidi,” Babu mtu alimwambia mjukuu wake, alishaelewa kuwa siku yoyote anaweza
kuaga dunia.
Huu ni mwanzo tu,
hadithi ndiyo kwanza inaanza. Fuatilia ujue Masato amefanya mambo gani? Usikose
kusoma kitabu changu cha WANAWAKE WAZURI MATESO, kinauzwa TSH 4000/= Kwa wauzaji wa magazeti nchi nzima.
Jumatatu, 25 Agosti 2014
MKASA WA KWELI
NYUMBA NDOGO ILIVYOVUNJA NDOA YANGU (1)
Kilikuwa chumba kidogo chenye vikirokoro vingi
vya vyombo, viatu, kabati la nguo, jiko, mafurushi ya nguo na meza ya chakula.
Chumba hiki kilimilikiwa na Willbroad
Masumbuko, aliyekuwa akiishi na mkewe aitwaye Vumilia. Ukweli, si kwamba
mwanaume huyu alishindwa kujenga nyumba, lahashaa. Kazi yake ilikuwa
ikimuingizia kipato kikubwa sana cha kuweza kuwa na hata vyumba viwili, sema
aliegemea upande wa ulevi na wanawake wengine.
Kazi yake ya udereva wa malori yaliyokuwa
yakifanya safari zake za Congo, Zambia, Malawi, Uganda na Zimbabwe ilimfanya
apate pesa nyingi. Willbroad hakuwa na huruma, usiku mzima alikuwa akisumbuana
na mkewe, kwa kumtaka mapenzi.
Vumilia alikuwa akihangaika, tumbo la uzazi
lilikuwa likimkata si kidogo. Maumivu ya uchungu yalimfanya alie sana, lakini
mumewe hakujali kama mkewe ujauzito wake ulikuwa umefika muda wa kujifungua,
siku hii alichokuwa akitaka ni mapenzi tu.
“Vumilia, huwezi kuninyima mapenzi, nipe
nitanue njia…nimekaa Congo mwezi mzima, ulikuwa na mwanaume gani unayempa
mapenzi?”
“Sina mwanaume mume wangu, sijawahi kufikiria
kukusaliti…nionee huruma siwezi kukupa penzi kwa sasa mume wangu, tumbo
linaniuma sana…”
“Linakuumaje ? Acha utani, nipe mapenzi…”
Willbroad aliendelea kutumia nguvu ili kupata penzi.
“Utaniua mume wangu, usinibake…tutamuua mtoto
wetu…” Vumilia alijaribu kumzuia mumewe asiweze kumbaka, ikashindikana.
Willbroad Masumbuko, mwenye nguvu nyingi aliendelea kumng’an’gania mkewe ili
amalize haja zake. Hakufikiria maumivu aliyokuwa akipata mkewe, hakujali kwamba
mkewe anasumbuliwa na uchungu wa uzazi aliendelea kumtanua miguu na kuingia
katikati ya miguu akijiandaa kumuingilia kimwili.
“Mume wangu, nionee huruma, utaniua
bure…vumilia nikijifungua nitakupa tu, kwanini unaning’ang’aniza mapenzi…”
“Sasa unafikiri nilikuoa ili ufanyeje? Ndoa
imekushinda?”
“Haijanishinda, uliza hata wanaume wenzako.
Mwanamke akiwa mjamzito anayetakiwa kujifungua leo anafanywaje? Ungekuwa na
somo juu ya uzazi ungenionea huruma, natamani nikuhamishie maumivu ya uchungu,
hakika ungeniacha…najua umenioa ili nikutunze, nivumilie, naumia mume
wangu...tumbo linauma…,” alisema maneno hayo Vumilia akizidi kuangua kilio.
Mumewe aliyekuwa na roho ya kinyama, hakujali sauti wala kilio chake . Maungoni
alisisimka kweli kweli na hapo ndipo akamalizia kufungua kufuli na kuanza
kumuingilia mkewe wakati anasumbuliwa na uchungu wa uzazi. Mfuko wa uzazi
(chupa) lilishapasuka na hali ilikuwa ni ngumu sana kwa Vumilia kuweza
kuvumilia.
“Naona umeamua kuniua mume wangu…”
“Sikuui, uliitaka ndoa..acha unipe haki
zangu…”
“Najua ni haki zako, ila huna huruma…huna
uvumilivu wa ndoa…kama ndoa zote zipo hivyo basi, itabidi niombe talaka…”
“Talaka sitoi, sijui kuacha, najua
kuoa…tulia…,” alipoona ugomvi umezidi, Vumilia akaanza kuangua kilio kwa sauti
ya juu, mumewe akamnasa kibao cha shavuni, akanyamaza kidogo huku machozi
yakimtirirka mashavuni na milio ya kwikwi ikasikika.
“Niue tu…unizike…,” alisema Vumilia kwa tabu,
huku jasho likimtoka mwili mzima.
Katika kufanyiwa ukatili huo, alijikuta
akihisi kuishiwa nguvu. Mumewe hakujali, aliendelea kumuingilia kimwili hadi
alipomaliza haja zake na kumuacha amelala hoi kitandani.
“Pole sana, sasa ngoja niende kazini, kuna
kontena naenda kupakia kisha nirudi Congo…nitakuja jioni kujua
unaendeleaje…”Willbroad Masumbuko alisema na kumwachia mkewe shilingi elfu tano
za matumizi ya siku hiyo.
“Mume wangu, sina pesa nyingine…hizo hazitoshi
kwenda hospitalini, si unajua hali yangu jamani…”
“Hazikutoshi, unataka kiasi gani?”
“Yoyote inayofaa, hata elfu ishirini, hivi
unajua hata vifaa vya kujifungulia sijanunua…”
“Kwani vinauzwa, si unaenda kujifungua
hospitali za serikali?”
“Ndiyo, lazima niwe na vifaa….kama pamba,
gloves na pesa zingine za dawa…”
“Wewe nenda, utanipigia simu…” alijibu
Masumbuko na kutoka.
Alimuacha mkewe aliendelea kuangua kilio,
juhudi za kuomba aongezewe pesa ziligoma. Afanyaje?
Dakika moja baadaye, Willbroad alirejea,
“Nimesahau, naomba uniazime simu yako…”
“Mume wangu simu hii nitaitumia kwa
mawasiliano, hali yangu si nzuri, nataka niwapigie ndugu zangu…”
“Wewe nipe nitawapigia…” aliichukua simu ya
mkwe na kutoka.
Bila huruma, Masumbuko aliondoka zake na
kurudishia mlango.
*****
Vumilia alishindwa kujizuia, uchungu uliendelea
kumsumbua, ukizingatia walikuwa wakiishi Mwananyamala A, nyumba ya kupanga.
Alipoona hana msaada, alijaribu kuinuka kitandani kwa tabu sana huku amebana
miguu ili mtoto asiweze kutoka. Haja kubwa ilikuwa inamsumbua, lakini akahisi
akiingia msalani mtoto angeweza kutumbukia chooni.
Alitembea kwa kushikilia ukuta hadi kufanikiwa
kutoka nje.
“Jamani nikoeni, nakufa sasa…”
“Vumilia, una tatizo gani?”
“Uchungu, naomba mnipeleke hospitali, mtoto
anataka kutoka…”
“Basi, ngoja tutafute usafiri…” Mama Amina,
jirani wa Vumilia alisema, alitoka akikimbia hadi kituo cha teksi, akaongea na
dereva teksi kwa ajili ya kumuwahisha mwanamke huyo hospitali.
“Mumewe yupo wapi?” dereva teksi alisema.
“Kandoka, yaani mwanaume hamjali mkewe ni hawa
madereva wa malori, sijui ni mtu wa aina gani?”
“Mpumbavu sana, sasa kwanini alimuoa?”
“Hata sijui, mwanaume mwenyewe katili kweli,”
alisema Mama Amina.
Walipofika nyumbani kwa Vumilia, waliegesha
gari nje na kumchukua wakamuwahisha hospitalini ya Mwananyamala, walimpokea na kuwambia
itabidi apelekwe Muhimbili.
*****
Chumba cha upasuaji hospitali ya Taifa
Muhimbili, kulikuwa na wanawake kumi waliokuwa akijifungua wakati huo. Mmoja wa
wazazi waliokuwa wakijitahidi kusukuma mtoto alikuwa Vumilia Jorome. Jasho
lilizidi kumtoka huku akihangaika na madaktari wakijaribu kumsaidia ingawa
ilishindikana.
“Kwanza, mbona kuna mbegu za kiume humu…”
“Mume wangu alikuwa akinilazimisha mapenzi…”
“Mpumbavu sana. Yupo wapi?”
“Hayupo, ameondoka na kunitelekeza…”
“Kweli, ni mumeo au hawara…”
“Mume wangu…” Vumilia alizidi kuangua kilio cha
uchungu.
“Mtoto amekaa vibaya, sasa ili kuweza kuokoa
uhai wake na mtoto itabidi ufanyiwe upasuaji haraka iwezekanavyo…” Dokta Kim
alimweleza daktari mwenzake.
“Ni kweli, maana hata hivyo njia ya binti
huyu ni ndogo…”
“Kweli, itabidi afanyiwe upasuaji…”
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)